Zawadi Tosha
Ordinary Time,MarianThanksgiving
Chorus
Nimetunukiwa tuzo lenye thamani
Nimeletewa zawadi toka mbinguni
Nimejishindia Mwana wa Mungu
Nimepewa Yesu zawadi tosha
Verse 2
Ninashangilia naimba kwa furaha
Ninarukaruka nacheza kwa furaha
Napiga makofi na vigelegele
Nimempata Yesu tuzo la ajabu (mimi)
Verse 3
Ninakushukuru ee Mungu Baba yetu
Nasema asante kwa mema yako yote
Napiga filimbi, ngoma na kayamba
Nimejishindia Bwana wa mabwana
Verse 4
Nikiwa na Yesu, magonjwa yamepona
Nikiwa na Yesu mashaka yamekwisha
Yesu kiongozi, Yesu Jemedari
Yesu mchungaji, Yesu mambo yote
Verse 5
Maisha marefu ni tuzo nimetuzwa
Uzima milele nimeshaahidiwa
Mbinguni kwa Baba nitakaribishwa
Nitaishi vyema siku zangu zote