Verse 1
Zanena, siku kuu,
Kengele za juu,
Waumini furahini,
Mkombozi mkumbusheni
Mzawa leo Bethlehemu
Mzawa leo Bethlehemu
Verse 2
Ni hii leo, siku heri,
Siku nzuri nzuri,
Ya uasi kuondolewa,
Ya mbingu kufunguliwa
Yakisha maulaumu,
Yakisha malaumu
Verse 3
Ni hii leo, siku njema,
Siku ya salama,
Aliposhuka Mwokozi,
Mwanaye Mungu Mwenyezi
Kuwa mwanadamu,
Kuwa mwanadamun
Verse 4
Leo siku, hakika,
Wala hamna shaka
Kwamba dhambi ya asili,
Yaweza kufutwa kweli
Ina dawa timamu,
Ina dawa timamun
Verse 5
Leo siku ya neema,
Yameshuka mema
Asifiwe Mungu juu,
Watu wa imani kuu
Waletewa amani,
Waletewa amani