Yesu Ni Mwema

Ordinary Time,MarianThanksgiving
Verse 1

Nimetafakari habari zako nami nashindwa kuelewa kabisa

Binadamu angenipa neema kesho angechoka kunipa zaidi

Lakini wewe hauna kikomo, wala mvua yako haina majira

Bwana, wanyesha mvua, Bwana, kwa walio jangwani

Bwana, wawasha jua, Bwana, mpaka baharini

Kweli Bwana wewe ni mwema sana

Chorus

Nitasimulia miji, Yesu ni mwema, Yesu ni mwema

Nitahubiri vijini, Yesu ni mwema Yesu ni mwema

Nitayafafanua haya, Yesu ni mwema Yesu ni mwema

Watu wote wapate kuyajua, Yesu ni mwema Yesu ni mwema

Nitasimulia nchi, Yesu ni mwema Yesu ni mwema

Verse 3

Niliwaza kwa ubinadamu mpaka mwisho wa kufikiri

Ukataka nijipe moyo, nisihofu kitu

Kwa kuwa humtupi anayekutumainia

Ukataka nijipe moyo, nisihofu kitu, kamwe

Verse 4

Uzoefu wa mapito haya ukaninyima usingizi

Ukataka nijipe moyo, nisihofu kitu

Kanuni za dunia zikavunja matumaini

Ukataka nijipe moyo, nisihofu kitu, kamwe

Verse 5

Giza lilipotanda mchana likanifunika usoni

Ukataka nijipe moyo, nisihofu kitu

Nikapiga kelele hofu kuu ikanisonga

Ukataka nijipe moyo, nisihofu kitu, kamwen

Verse 6

n< h i t i m i s h o>nn[t|b] Naimba he he, naimba leo

Naimba he he, naimba mimi

Ulijua wazi kwamba mimi sikuwa nastahili,

Kwa sababu mimi mdhaifu mwili na roho

Ukaruhusu nifanikiwe juhudi zangu

Makusudi ili nione ukuu wako

Ndugu wanipende, jamaa waniheshimu

Marafiki wanijali, wanisaidie

Ndiyo maana leo, mimi nakurudishia;n

Verse 7

n[w] Utukufu ni wako milele

Sifa heshima ni vyako daima

Wewe peke yako unastahili

Usifiwe na uhimidiwe!

Verse 8

Nakushukuru Bwana, kwa kuwa umeniona asante

Nakushukuru Bwana, kwa kuwa umeniona asante

Nakupa utukufu, kwa kuwa umeniona asante

Milele na milele, kwa kuwa umeniona asante

Nakushukuru Bwana, kwa kuwa umeniona asanten