SectionsEucharistYesu Mwema Najitolea Kwako

Yesu Mwema Najitolea Kwako

Ordinary Time,MarianEucharist
Verse 1

Yesu mwema najitolea kwako,

Kwa leo hii na siku zote

Nafsi yangu na moyo wangu wote

Heri kweli, heri kweli, heri kweli raha ya uwingu *2

Verse 2

Ndani mwangu umekuja daima,

Kuwa nami ni pendo lako

Ewe mpenzi mwenye utamu mwingi

Ni mapendo, ni mapendo, ni mapendo ya moyo wako *2

Verse 3

Nitaweza kukurudishia nini,

Kwa wema huu na pendo lako

Roho yangu umeifadhilia

Nikupende, nikupende, nikupende ni tamaa yangu*2n

Verse 4

Weka Rabi katika roho yangu,

Wema wako na unyenyekevu,

Na pendo kuu fadhila ya imani

Niongoze, niongoze, niongoze katika imani *2n