Verse 1
Yesu mwema najitolea kwako,
Kwa leo hii na siku zote
Nafsi yangu na moyo wangu wote
Heri kweli, heri kweli, heri kweli raha ya uwingu *2
Verse 2
Ndani mwangu umekuja daima,
Kuwa nami ni pendo lako
Ewe mpenzi mwenye utamu mwingi
Ni mapendo, ni mapendo, ni mapendo ya moyo wako *2
Verse 3
Nitaweza kukurudishia nini,
Kwa wema huu na pendo lako
Roho yangu umeifadhilia
Nikupende, nikupende, nikupende ni tamaa yangu*2n
Verse 4
Weka Rabi katika roho yangu,
Wema wako na unyenyekevu,
Na pendo kuu fadhila ya imani
Niongoze, niongoze, niongoze katika imani *2n