Verse 1
Tunapoona Bwana Yesu kuteswa msalabani
Tunasikitika kweli
Kwani tumekusulubu ee Bwana utuhurumie
Verse 2
Dhambi zetu nyingi sana asili ya mateso
Watupenda mpaka mwisho
Umekufa tuokoke ee Bwana utuhurumie
Verse 3
Tunapona msalabani sawa na mwizi mbaya
Ulitaka kutukanya
Tuyaache majivuno, ee Bwana utuhurumie
Verse 4
Tunapoona msalabani miiba yachoma kichwa
Unalipa kwa matesa
Fungua na tamaa zetu ee Bwana utuhurumie
Verse 5
Msalabani, umefungwa na mikono ya damu
Mkono wako wenye heri
Utujaze na baraka, ee Bwana utuhurumie
Verse 6
Mwili wote wafunikwa, na damu ivujayo
Damu yako isafishe
Uovu wote wa rohoni, ee Bwana utuhurumie
Verse 7
Moyo wako umetonwa, mlango sasa wazi
Tutakase tuingie,
Tukae moyoni mwako, ee Bwana utuhurumie