Wosia

Ordinary Time,MarianExit
Verse 1

Tulieni ndugu zangu niwaambie siri moja

Mkimtumainia Mungu mtayashinda yote

Japo magumu ni mengi mtakayokutana nayo

Mkimtumainia Mungu mtayashinda yote

Chorus

{ Mtavuka vikwazo vya shetani na magumu yote (nasema)

Mbinu zake shetani na hila hazitawaangusha (nasema)

Mkimtumainia Mungu mtayashinda yote } *2

Verse 3

Kwa nguvu za Mwenyezi nasema hamtaaibika-

Mtautimiza huu wito wenu kikamilifu -

Verse 4

Mungu Baba yuko nyuma yenu anawapigania-

Atawafukuza na maadui wenye hila mbaya .

Verse 5

Wosia ninawapa ndugu muwe na uvumilivu-

Kwani haya ya dunia si kitu wala si lolote .