SectionsBible ProcessionWaumini Simameni

Waumini Simameni

Ordinary Time,MarianBible Procession
Verse 1

Waumini simameni - tupeleke neno lake

Neno lake Bwana Mungu - ni nuru ya ulimwengu *2

Chorus

Tulisome kweli (kweli kweli)

Tulihubiri sana(biri sana)

Tulisambaze kote na tulifundishe kweli

Chorus

Tulisome kweli (kweli kweli)

Tulihubiri sana(biri sana)

Tulisambaze kote na tulifundishe

Verse 4

Ni neno la Bibilia - kutoka kwa Mungu Baba

Anena kwa kinywa chake - na kwa maandiko yake *2n

Verse 5

Ni dawa ya mioyo yetu - tulizo kwa watu wote

Tulipokeeni leo - tupate kunusurika *2n

Verse 6

Tuchezeni kwa furaha - nderemo na kwa vifijo

Kwa ngoma na tarumbeta - kayamba hata vinanda

Verse 7

Milima iyumbeyumbe - miti na ichezecheze

Bahari ivume sana - mito ipige makofi *2