SectionsEucharistWatumishi Wake Baba

Watumishi Wake Baba

Lent,LentEucharist
Verse 1

Watumishi wake Baba wangapi waliopo

Wanakula na kusaza chakula chake Baba.

Chorus

Nami - Nami nataabika hapa,

Nashi - Nashiriki na nguruwe,

Chaku - Chakula kisichofaa, yanipasa kurudi

Nita - Nitarudi na kusema,

Baba - Baba yangu nisamehe,

Nime - Nimekosa kwake Mungu,nna mbele yako, Baba.

Verse 3

Baba kamuona yu mbali,nkashikwa na huruma:

Akakimbia kumlaki, kamkumbata na busu

Verse 4

Baba sistahili tena kuitwa mwana wako;

Unifanye kama mmoja wa watumishi wako.

Verse 5

Baba yangu, nimekosa, ninaomba huruma;nunisamehe, nirudi, nikakutumikie.

Verse 6

Nasogea ninakuja, ninakukimbilia,

Mimi ni mtoto mpotevu, Baba unipokee.

Verse 7

Wanikaribisha mimi kwenye karamu yako,nmeza imeandaliwa, inaningoja mimi.