SectionsExitWatu Hawatalingana

Watu Hawatalingana

Ordinary TimeExit
Verse 1

{Watu hawatalingana (daima), watatofautianan(nayo ni) makusudi yake Mungu, jina lake litukuzwe } *3

Chorus

{ Sote tumeumbika tulivyo (kadiri) ya mapenzi yake Mungu

Ili utukufu wake Mungu (Mwenyezi) ujulikane kwa wote } *2

Verse 3

Kweli wanadamu wote (hakika) tumeumbwa kwa udongon(hivyo) asili yetu ni moja, tumetoka mavumbini

Verse 4

Wapo walio wanyonge (lakini), pia wapo wenye nguvun(kusudi) Mungu kawaumba hivyo, ili wahudumiane

Verse 5

Wengine kawabariki (sana), amewajalia malin(lakini) wengine amewashusha, wamekuwa hohe hahe.

Verse 6

Wale walio tajiri (kamwe), wasiwanyime fukaran(kwani) maskini wahitaji, huruma ya matajiri

Verse 7

Wote tu wana wa Mungu (hivyo) tuonyeshane upendon(ili) Mungu wetu atukuzwe, sasa na hata milele.