Verse 1
Wakristu wote simameni, simameni
Tuchezeni mbele za Bwana, kwa shukrani
Chorus
(Leo) Asubuhi na mchana nitamsifu (Bwana)
Na usiku nitaita jina la Bwana (wangu)
Sifa zake zi kinywani mwangu daima
Nitaimba sifa zake Mungu milele
Verse 3
Tupeperusheni mikono juu hewani
Tushangilieni tupigeni makofi
Verse 4
Ametulisha kwa chakula cha mbinguni
Twaburudika kwa kinywaji cha uzima
Verse 5
Ametukinga na maovu ya dunia
Mapenzi yake kwetu sisi ni ya ajabu
Verse 6
Turukeruke na tucheze kama ndama
Tupigeni ngoma kayamba na vinanda