Chorus
{ Wakati sasa umeshafika wa kujifikiria
Kitu gani umtolee Bwana kama shukrani zako } *2n{ Toa kwa moyo wa mapendo,
Toa ulicho nacho (ndugu) toa kwa ukarimu
Mungu anakuona ndugu mpaka moyoni mwako } *2
Verse 2
Ewe ndugu usimame, nenda mbele zake Bwana
Kamtolee sadaka Bwana kwa mapendo yote
Verse 3
Tolea moyo wako, pamoja na matendo yako
Naye Bwana Mungu wako kweli atakubariki
Verse 4
Siku zote Mungu wako amekulinda vyema
Nawe sasa ndugu yangu hima ujifikirie
Verse 5
Baraka zake Mungu za Baba na za Mwana
Na za Roho Mtakatifu ziwe nanyi siku zote