SectionsOffertoryUtukuzwe Ewe Bwana

Utukuzwe Ewe Bwana

Ordinary Time,MarianOffertory
Verse 1

Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya

Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya

Chorus

Utukuzwe - utukuzwe

Baba Muumba ulimwengu - aleluya

Verse 3

Tumepokea mkate, mazao ya mashamba, aleluya

Ndio alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya

Verse 4

Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya

Jalie uwe kwetu, chakula cha uzima, aleluya

Verse 5

Zawadi ya divai, kutoka mzabibu, aleluya

Ndiyo alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya

Verse 6

Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya

Jalie iwe kwetu, kinywaji cha kiroho, aleluya

Verse 7

Sifa kwako ee Mungu uliyetuchagua, aleluya

Shukrani kwako Baba, kwa kutulisha sisi, aleluya

Verse 8

Kwa pendo na fadhili, umetufurahisha, aleluya

Ukatufikisha kwa sherehe yetu leo, aleluya

Verse 9

Siku ya leo iwe kwa heshima na sifa, aleluya

Na utukufu wako na kwa mafaa yako, aleluya