Verse 1
Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya
Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe, aleluya
Chorus
Utukuzwe - utukuzwe
Baba Muumba ulimwengu - aleluya
Verse 3
Tumepokea mkate, mazao ya mashamba, aleluya
Ndio alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya
Verse 4
Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya
Jalie uwe kwetu, chakula cha uzima, aleluya
Verse 5
Zawadi ya divai, kutoka mzabibu, aleluya
Ndiyo alama kwetu, ya wema wako mkuu, aleluya
Verse 6
Ni tunda la bidii, ya mkono na ya moyo, aleluya
Jalie iwe kwetu, kinywaji cha kiroho, aleluya
Verse 7
Sifa kwako ee Mungu uliyetuchagua, aleluya
Shukrani kwako Baba, kwa kutulisha sisi, aleluya
Verse 8
Kwa pendo na fadhili, umetufurahisha, aleluya
Ukatufikisha kwa sherehe yetu leo, aleluya
Verse 9
Siku ya leo iwe kwa heshima na sifa, aleluya
Na utukufu wako na kwa mafaa yako, aleluya