SectionsEucharistUtukufu (Migori)

Utukufu (Migori)

Ordinary Time,MarianEucharist
Chorus

Utukufu kwa Mungu juu

Na amani duniani

Na amani kwa watu woten{Wenye - wenye mapenzi,

Watu - wenye mapenzi

Mema - wenye mapenzi

Watu - wenye mapenzi mema }*2

Verse 2

Tunakusifu tunakuheshimu

Tunakuabudu tunakutukuza

Tunakushukuru kwa ajili ya

Utukufu wako, wako mkuu

Verse 3

Ee Bwana Mungu mfalme wa mbinguni,

Mungu Baba mwenyezi ee Bwana Yesu Kristu

Mwana wa pekee ee mwana Mungu

Mwanakondoo wa Mungu, mwana wa Baba

Verse 4

Mwenye kuondoa dhambi za dunia

Ewe mwenye kuondoa dhambi za dunia

Pokea ombi letu ewe mwenye kuketi

Kuume kwa Baba, utuhurumien

Verse 5

Kwa kuwa ndiwe uliye peke yako

Peke yako mkuu ee Bwana Yesu Kristu

Pamoja na roho mtakatifu

Katika utukufu, wa Mungu Baba amina