Chorus
Utukufu juu kwa Mungu, Utukufu juu Mbinguni
Na amani kote duniani, Kwa wenye mapenzi mema
Verse 2
Tunakusifu tunakuheshimu, tunakuabu tunakutukuza
Twakushukuru kwa ajili, ya utukufu wako mkuu
Verse 3
Ewe Mungu ndiye mfalme, wa mbinguni Baba mwenyezi
Ewe Bwana Yesu Kristu, wa pekee mwana wa baba
Verse 4
Ewe Yesu mwanakondoo, wa Mungu mwana wa Baba
Ewe mwenye kuziondoa, dhambi zetu tuhurumie
Verse 5
Ewe mwenye kuziondoa, za dunia dhambi za watu
Ewe mwenye rehema nyingi, upokee maombi yetun
Verse 6
Uketiye kuume kwake, Mungu Baba tuhurumie
Kwa kuwa ndiwe uliye, peke yako Mtakatifu
Verse 7
Peke yako ni wewe Bwana, peke yako Bwana mkuu
Peke yako ni mkombozi, peke yako Yesu Kristun
Verse 8
Naye Roho Mtakatifu, katika utukufu wake
Mungu mmoja anayeishi, na kutawala milele yote.n