Ee Mwenyezi Mungu utanisahau kabisa mpaka lini?
Utauficha uso wako mbali nami mpaka lini Mungu wangu?
Roho na mwili wangu vitakuwa na wasiwasi mpaka lini?
Na masikitiko siku hata siku sina raha maishani
Bwana nimelia sana, mchana uko wapi unifadhili
Na usiku usingizi sipati nakesha nikiwaza
Nimedhoofika sana fimbo kila siku nachapwa nimekonda
Sina pa kukimbilia njia zote zimelindwa niende wapin
Maadui zangu ni wengi, njaa magonjwa ya hatari na ajali
Vita vimepamba moto dunia yote ona Bwana ninavyotishwa
Ndugu na rafiki zangu wametoweka siwaoni wako wapi
Kama wako kwako Bwana nambie nami nijaribu kuwafuata
Yesu wangu u Mungu wangu njoo haraka nakuita njoo Bwana
Mwanao nateseka sijiwezi mimi ninaomba msaada wako
Ninainua mikono taabu mateso maumivu yangu yote
Ninakukabidhi wana yapokee Mwokozi naomba usinitype