Ushuhuda Tosha
Tuna haki ya kutamka na kutoa ushuhuda
Mambo mema alotenda Mungu pia na kwa huruma
Ninamwambia naye jirani Mungu ana huruma
{ Ushuhuda, huo ni ushuhuda tosha (nasema)
Ni huruma, Mungu ana huruma nyingi (hakika)
Ninapolala pia ninaamka huo wote ni ushuhuda tosha } *2
Kaumba mbingu na dunia wanyama hata samaki
Binadamu na akili nyingi sisi tukawatawale
Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
Tunalala bila kuomba hatimaye twaamka
Mungu wetu na hakasiriki bado atupa mkate
Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
Maisha yetu twayapanga nayo yanafanikiwa
Mara nyingi hata hatuombi kumshirikisha Mungu
Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
Tunapofanya biashara uongo tunatumia
Twazikiuka amri za Mungu ili tupate faida
Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
Ni mengi hatujatamka wanadamu tunafanya
Tunaomba msamaha Mungu sisi sote walegevu
Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu