Verse 1
Watu wengi tunajaribu upendo
Tunawajali wale wanaotuhusu
Tunaojua wataweza kutulipa
Hatuwathamini wale wasiotuhusu
Wala wasiojiweza, lakini
Chorus
{Leo tumejifunza wote,nupendo ni kitu gani (wapendwa)
Tena tumepewa mfano,nukarimu una sifa gani (wapenzi) } * 2n
Verse 3
Tunawakopesha wenye kipato kikubwa
Tukiamini nao watatukopesha
Wakitujia wenye shida na fukara
Tunawakimbia eti hawakopesheki
Na wana madeni mengi, lakini
Verse 4
Wakiugua wenye nafasi za juu
Tunajazana kwao na vichupachupa
Tukiamini na sisi tukiugua
Watalundikana kwetu na vifuko fuko
Kadi na michango mingi, lakini
Verse 5
Tukitembelewa na mtu mwenye viraka
Tunauliza kama tulimualika
Akija aliyeshuka kwenye shangingi
Tunamwuliza kinywaji anachokunywa
Tena kwa unyenyekevu lakini