Upendo Kupita Upeo
Ee Mungu wangu, kwa hakika unanipenda
Upeo wa macho yangu, sijui nikulipe nini
Maisha yangu, nayatazama nashukuru
Kwa yote uliyotenda, na pale uliponitoa
Ningelikuwa natazama ya binadamun(hakika leo) fadhila yake ingelikuwa madharau
Lakini wewe utoaye hewa na majin(watugawia) tajiri hata walemavu na maskini
Na marafiki, walinipenda wengi sana
Nilipokuwa na gari na nyumba yenye kupendeza
Walinipenda, pale pesa zilipoisha
Majuto niliyapata, nilipoachwa peke yangu
Maisha yangu, yalipokuwa yenye shida
Hakika ulinitoa, nilipoanguka shimoni
Baraka nyingi, ulimimina kwangu mimi
Hata nao majirani, sasa wamebaki butwaa
Ninashukuru, kwa kunikinga na ajali
Ninaposafiri mimi, umekuwa dereva wangu
Pia magonjwa, umeyapiga teke kwangu
Hakika nina sababu, ya kutamka sifa zako