SectionsEucharistUnivishe Pete

Univishe Pete

WeddingEucharist
Chorus

{ Ewe mwenzangu univishe pete kwenye chanda changu,

Iwe ni alama ya uaminifu wako } *2

Verse 2

Naapa mbele ya Mungu, mimi ni wako siku zote,

Nitamuacha Baba nitamwacha na mama

Niambatane nawe, nasi tutakuwa mwili mmoja

Verse 3

Wewe sio malaika ni mwanadamu kama mimi,

Makosa kawaida tuko sawa maumbile

Maumbile ya Mungu, nitakusamehe ukinikosea

Verse 4

Macho yangu yameona, yameona wengi sana,

Kati yao wengi, ninakuvika pete

Iwe alama yangu ya uaminifu wangu kwako