Chorus
Unioke uniokoe na watu hao wabaya
Na unikinge unikinge na wakatili
Wenye mawazo mabaya *2
Verse 2
Daima hao huzusha ugomvi
Na ndimi zao hatari kama nyoka
Midomo yao maneno hatari
Ni kama sumu hatari ya joka
Mwenyezi Mungu naomba unilinde
Kwa kucha zao wabaya na katili
Verse 3
Wenye kiburi hutega
Mipango yao waone uanguke
Wametandaza kamba kama wavu
Njiani wamezificha mitego
Mipango yao yote wanikamate
Sauti ya ombi langu sikiliza
Verse 4
Mkombozi mkuu wangu umenikinga
Salama hata wakati wa vita
Waovu usiwape wanayotataka
Mipango yao mibaya huivunje
Wameinua kucha wamenizingira
Uovu wao wenyewe uwapate