SectionsExitUmekosa Nini Yesu

Umekosa Nini Yesu

LentExit
Verse 1

Tuifuate Njia ya Msalaba, tuifuate mpaka Kalvari

Tusimamapo bila haya, (msalaba *2) huponya rohonn* * * * * *

Verse 2

Umekosa Nini we Yesu, kushtakiwa bure kwa Pilato

Wenye kustahili hukumu, si wewe, si wewe, Bwana ni sisi

Verse 3

Ole msalaba huo mzito, apagazwa Mwana Mpenzi wa Mungu

Mwili waenea mateso, alipa, alipa madhambi yetu

Verse 4

Ona Mumba Mbingu na nchi, yupo chini mzigo wamwelemea

Na mtu kiumbe chake kwa ukali, ampiga, ampiga bila huruma

Verse 5

Huko njiani we Maria, waonaje hali ya mwanao

Ni damu tupu na vidonda, machozi, machozi yamfumba macho

Verse 6

Kwa Simoni heri ya kweli, mimi pia Yesu nisaidie

Kuchukua mzigo wa ukombozi, kuteswa, kuteswa pamoja nawe

Verse 7

Uso wa Yesu malaika, Bethlehemu wakuabudu

Bahati yake Veronika, kupangusa, kupangusa mfalme wa mbingu

Verse 8

Wakimvuta huku na huku, wauaji wakamchokesha bure

Chini wamtupa bado kwa nguvu, aibu, aibu yao milele

Verse 9

Wanawake wa Israeli, msilie kwa sababu hiyo

Muwalilie hao kwa dhambi, upanga, upanga ni juu yao

Verse 10

Mwokozi sasa ni ya tatu, kuanguka chini ya msalaba

Katika dhambi za ulegevu, nijue, nijue kutubu hima

Verse 11

Muje malaika wa Mbingu, funikeni mwiliwe kwa huruma

Vidonda vyake na utupu, askari, askari wamvulia

Verse 12

Hapo mkristu ushike moyo, Bwana wako alazwa msalabani

Mara miguu na mikono, yafungwa, yafungwa kwa misumari

Verse 13

Yesu mpenzi nakuabudu, msalabani unapohangaika

Nchi yatetemeka kwa hofu, na jua, na jua linafifia

Verse 14

Mama Maria mtakatifu, upokee maiti ya mwanao

Tumemwua kwa dhambi zetu, twatubu, twatubu kwake na kwako

Verse 15

Pamoja naye kaburini, zika dhambi na ubaya wa moyo

Yesu tuwe wakristu wa kweli, twakupa, twakupa sasa mapendon

Verse 16

n* * * * * * * * *

Katika roho yangu Bwana, chora mateso niliyokutesa

Nisiyasahau madeni, na kazi, na kazi ya kuokoa