Uko Juu

Ordinary TimeExit
Verse 1

Hufanani nasi, unang'ara na tena una enzi, una utukufu

Umepita zote, sifa tunazokutolea sisi, nao malaika oho

Chorus

Wewe uko juu umetukuka na tunakuinua kwa nyimbo zetu hizi

Verse 3

Walikuimbia, baba zetu lakini hazikwisha, sifa zako wewe

Na watakatifu, wanaimba na hazimaliziki, tenzi hazitoshi oho

Verse 4

Mimea ya nchi, yaeleza inapopukutika, kuhifadhi maji

Kwamba wewe Bwana, hupungui unajua kuumba, hupitiwi neno oho

Verse 5

Kinyonga mdogo, anageuka rangi kujilinda, bila ya bunduki.

Anafafanua, umakini ndani ya kazi yako, isiyo dosari ohon

Verse 6

Na uhimidiwe, wewe Baba yaani ndiwe Mwana, Roho Mtukufu,

Ulivyotukuzwa, enzi zile sasa hata milele, utukuzwe pote ohon