SectionsEucharistUkaristia Ni Yesu

Ukaristia Ni Yesu

Ordinary Time,MarianEucharist
Verse 1

Ukaristia ni Yesu sadaka,

Ukaristia ni Yesu chakula,

Ukaristia ni mwili wa Yesu.

Verse 2

Ukaristia ni mkate wa Mungu,

Ukaristia ni mana ya kweli,

Ukaristia ni uzima wetu.

Verse 3

Ukaristia ni damu ya Yesu,

Ukaristia ni kinywaji chetu.

Ukaristia ni chem chem ya neema.

Verse 4

Yesu mwenyewe ametufundisha.

Yesu mwenyewe amefumbulia.

Neno la Mungu nani atakana?

Verse 5

Sogea meza yake takatifu,

Kwa moyo safi nawe umpokee,

Atatolea nyingi zake neema

Verse 6

Mungu mwamini, nakutumaini,

Ee Mungu mzima, ninakushukuru,

Ee Mungu wangu, nakupenda sana

Verse 7

Sadiki, mkristu, upate wokovu

Ndiyo ahadi ya Mwenyezi Mungu,

Mwisho mbinguni atakupokea