Verse 1
Uje Roho Mtakatifu, tuangaze toka mbingu
Roho zetu kwa mwangao
Verse 2
Uje Baba wa maskini, uje mtoa wa vipaji
Uje mwanga wa mioyo
Verse 3
Ee Mfariji mwema sana, ee rafiki mwanana
Ewe raha mustarehen
Verse 4
Kwenye kazi u pumziko, kwenye joto, burudiko
U mfutaji wa machozi
Verse 5
Ewe mwanga wenye heri, uwajaze waamini
Neema yako mioyoni
Verse 6
Bila nguvu yako wewe, mwanadamu hana kitu
Kwake yote yana kosa
Verse 7
Osha machafuko yetu, panyeshee pakavu petu
Na kuponya majerahan
Verse 8
Ulegeze ukaidi, washa moto wa uadili
Nyoosha upotevu wote
Verse 9
Wape waumini wako, wenye tumaini kwako
Paji zako zote saba
Verse 10
Wape tuzo ya fadhila, wape mwisho bila hila
Wape heri ya milele
Verse 11
Amina aleluya, amina aleluya,
Amina aleluya