SectionsExitUjana Ni Maji Moto

Ujana Ni Maji Moto

Ordinary TimeExit
Chorus

Ujana ni maji ya moto bila Mungu ni majuto

Ujana ni maji ya moto ukicheza utakuchoma

Kunapokucha ni raga

Mwili bado una nguvu nyingi

Tunapomsahau Mungu vijana twapotea *2

Verse 2

Vishawishi ni vingi mno, ili tupate pesa nyingi

Wengine tunaua ili tupate pesa

Twaharibu amani ili tupate pesa

Tunapomsahau Mungu vijana twapotea

Verse 3

Magaidi wanatutumia, twauana sisi kwa sisi

Jamii inalia machozi ya uchungu

Wasio na hatia wauawa kwa nini

Tunapomsahau Mungu vijana twapotea

Verse 4

Ndoto zetu zinakatizwa, na wale wasio na utu

Wasiwasi kazini, wasiwasi shuleni

Mjini wasiwasi twatembea kwa hofu

Tunapomsahau Mungu vijana twapotea