//utangulizin
Ninyi mliitwa ndugu muwe watu huru kabisa
Lakini uhuru huo sio wa kuusingizia
Isiwe ni sababu - ya kutawaliwa na tamaa hizi
Tamaa za dunia - msitawaliwe na tamaa za dunia
Ooh jifunzeni kutumikiana kwa upendo daima
Kwani sheria ni moja nayo ndiyo upendo
n//kiitikio
Uhuru wangu ee - uhuru wangu
Uhuru wangu wa thamani
Uhuru wangu jamani - uhuru wangu (uhuru)
Unatokana na ukweli
Nikijisifu kwa uongo, nateseka
Kwani siwezi dhihirisha sifa yenyewe
Jamii itatarajia kutoka kwangu
Nisiyoweza kuyatenda, kwani si ya kweli!
Nikifanya udanganyifu, kwenye fedha
Nikimwona ausikaye ninazizima
Au nikipokea rushwa, nitanena
Hata yale yasiyo mema, yanidhalilishe!
Nikikosa uaminifu, kwenye ndoa
Nitakwepa kuongozana, na mpendwa wangu
Ili tusije kukutana, na hawara
Akashindwa kuvumilia, akanipondeza!
Nikizunguka nchi nzima, kuongea
Uwogo juu ya mwenzangu, najiumiza
Tukikutana ana njaa, yuko kimya
Nitadhani wamemwambia, nitapata hofu
Nikimtesa mpwa wangu, nimleaye
Sitatamani aonane na wazazi wake
Kwani najua atasema, nimtendeayo
Na mimi nitadhalilika, nitaaibika!
Nikifanya upendeleo, ofisini
Kumkweza asiyefaa, najidhihaki
Jamii ikimhubiri, afaaye
Nitahisi nakejeliwa na kuunguliwan
n// hitimishon---
Kwa sababu mimi, ndiye, ninaiandika mwenyewe
Historia yangu, leo, itakayosomwa milele
Daima milele, daima milele, daima milele
Muamuzi wangu ndimi!