Uhimidiwe
Ordinary Time,MarianThanksgiving
Verse 1
Nakutumaini wewe Mungu wa huruma
Naitumaini damu yako ilojaa upendo
Ninakuhimidi Bwana nakupenda sana
Ninakuhimidi Bwana Yesu maishani mwangu
Chorus
Uhimidiwe - uhimidiwe wewe Bwana uhimidiwe *2
Unanipenda - uhimidiwe
Unanijali - uhimidiwe
Unasamehe - uhimidiwe na kutukuzwa aee
Verse 3
Kila ifikapo kumekucha mimi naamka
Riziki mtaani Bwana mimi natafuta
Chochote kila unanipa
Na hata kama ninakosa
Tamaa mimi sitokata
Uhimidiwe ee Bwana Yesu
Verse 4
Tazama na watoto yatima wanakulilia
Nao mama wajane nao wakusubiria
Tazama nao wazee
Tazama nao wafungwa
Tazama nao wagonjwa
Uhimidiwe ee Bwana Yesu
Verse 5
Oo Tuserebuke - tuserebuke tumtangaze ahimidiwe *2
Tuserebuke kwa shangwe na tuserebukenpamoja na tuserebuke ahimidiwe
Dunia nzima tuserebuke tumtangaze huyoo