SectionsExitUfurahi Moyo Wao (Ii)

Ufurahi Moyo Wao (Ii)

Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,MarianExit
Chorus

Ufurahi moyo wao, wamtafutao Bwana *2n{ Mtafuteni Bwana, na nguvu zake

Utafuteni uso wake siku zote } *2

Verse 2

Kwa nyimbo nzuri na ngoma tamu, kwa vinubi pia vinanda,

Tupige makofi tumtukuze Mungu mwenye uwezo

Mshangilieni, mwimbieni Bwana

Usimulieni ukuu wake siku kwa siku

Verse 3

Simameni wababa wote, inukeni na kina mama

Vijana wacheze na watoto warukeruke leo

Msifuni Mungu, mwabuduni Yeye,

Tafuteni Bwana maana anapatikana

Verse 4

Lisifieni jina takatifu, nyanyukeni viumbe vyote

Zikumbukeni ajabu na hukumu ya kinywa chake

Msifuni Mungu, mwabuduni yeye

Mwambieni Yahweh, matendo yake yanatisha

Verse 5

Mshukuruni Mwenyezi Mungu, tangazeni ukuu wake

Yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda

Mshangilieni, mwambieni Bwana

Msimulieni matendo yake ya ajabu.