SectionsOffertoryTwaja Kwako Bwana

Twaja Kwako Bwana

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary TimeOffertory
Chorus

Twaja kwako Bwana (leo) kwa furaha kubwa (sisi)

Twaleta zawadi Bwana tukushukuru

Kwa Baraka zako (zote) nayo mema yako (kwetu)

Kweli u mkarimu Bwana masihani mwetu.

Chorus

Twajitoa kwako, Bwana utupokee sisi

Japo hatustahili, twaja ututakase

Nafsi zetu sisi, twazitoa kwako ee Bwana

Ili iwe ishara, ya shukrani zetu kwako

Verse 3

Mkate mazao ya ngano, tunakutolea Bwana

Upate kugeuza uwe mwili wako Bwana.

Kutoka kwa mizabibu tunaleta na divai, Bwana uigeuze

Iwe kinywaji cha roho, tupate uzima wako

Verse 4

Kutoka kwa mifuko yetu, tunakutolea fedha

Kama fungu la kumi, Bwana zibariki zote

Kutokana na bidii zetu tunakutolea mazao ya mashamba

Kutoka kwa boma zetu, twaleta mifugo kwako

Verse 5

Tunajitoa kwako Bwana kwa nafsi na maisha yetu,

Pia na nguvu zetu tuwe watumishi wako

Mioyo yetu twaleta kwako tupokee Bwana, sisi ni waja wako

Tutumie jinsi wewe utakavyopenda Bwana.n

Verse 6

Zawadi tuletazo kwako kwa moyo wa ukarimu

Tunakuomba Bwana nazo zipokee kwako

Utujalie Baraka pia na fadhili zako, wewe ni Mungu wetu

Nasi tutaishi daima ndani yako Baba yetu