Chorus
Tutaishia kusema hii dunia mbaya (kweli) * 2
Mungu kaikamilisha bila kusahau kitu sasa
Dunia iweje mbaya kwa sababu ya walimwengu
Verse 2
Mungu kaumba dunia kwa mpango kamilifu
Kuhakikisha usalama kwa kila alichokiumba
Mazao yanastawi chakula kinatutosha, na mvuanzinanyesha sana kwa sababu ya upendo wake
Verse 3
Wapo walio fukara ambao hawajiwezi
Matajiri hawawasaidii japo wana uwezo
Pia mahospitalini hongo zimeshatawala
Pesa sasa zinatawala kuliko upendo wa Mungun
Verse 4
Viongozi maofisini wananyanyasa raia
Bila hongo hakuna kazi ubinadamu uko wapi
Dunia hii ya leo imetapakaa damu
Silaha za kutisha sana kutwa kucha zafanya kazin