SectionsEntranceTunasonga Mbele

Tunasonga Mbele

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Verse 1

Ingawaje ni mbali sana, mbinguni penye makao mazuri

Lakini tunapatamani, tutafika na tutaishi milele

Ina milima na mabonde, njia inayoelekea huko

Lakini tunajitahidi, hatusitishwi, hatukati tamaa aya aya hee

Chorus

Tunakanyaga, tunasonga hatulali

Tunakwenda, tunasonga hatulali

Polepole, tunasonga hatulali

Taratibu, tunasonga hatulali }* 2

Verse 3

Kanuni tumezisikia, na tunajitahidi kuzishika,

Tukiteleza twainuka, hatulali na hatufungi ukope

Kuwapenda jirani zetu kupoteza kusudi wafaidi

Kama Yesu alivyofanya, akakuja na kufa msalabani aya aya hee

Verse 4

Hatutakwi kuzubaa, dunia siyo makao yetu

Tumeletwa kutumikia, kuondoka na kurudi kwake Mungu

Iwe isiwe tutafika, kwa sababu njiani ni kweupe

Kulisafishwa Kalvari, hakika tu ni kupita bila shaka aya aya hee