SectionsSign of PeaceTunaishi Kwa Amani

Tunaishi Kwa Amani

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeSign of Peace
Chorus

(Tunaishi pamoja kwa amani ee ndugu yangu,

Kama jumuiya moja, kwa pendo la Mungu *2)

Ona, {Tumeunganishwa (sote)

Kwa pendo lake Muumba, Sasa,nkwa nini tufarakane

Kwa mambo yatutengayo na Mungu }*2

Verse 2

Ugomvi kati yetu unatoka wapi,

Mbona sisi sote ni watoto wa Baba mmoja

Kwa nini tugombee mali za dunia

Tukumbuke pendo lake Mungu, tuondoe tofauti zetu

Verse 3

We baba nawe mama mwagombea nini

Mbona mwasahau ahadi yenu siku ya ndoa

Ugomvi wenu unaathiri watoto

Kumbukeni pendo lake Mungu, muondoe tofauti zenu

Verse 4

Makasisi, watawa mwatafuta nini

Mbona mwasahau ahadi nazo nadhiri zenu

Ubinadamu mbona unawatawala

Kumbukeni pendo lake Mungu, m'mkabidhi maisha yenu,

Verse 5

Ugomvi wa kidini unatoka wapi

Mbona sisi sote ni raiya wa taifa moja,

Kubagua kabila, rangi ni kwa nini

Tukumbuke pendo lake Mungu, tuondoe tofauti zetu

Verse 6

Sasa enyi vijana mwatafuta nini

Mbona matendo yenu mengi ni chukizo kwa Mungu,

Hamuheshimu wazazi na Mungu wenu

Kumbukeni pendo lake Mungu, m'mrudieni Mungu wenu