SectionsExitTumuogope Mungu

Tumuogope Mungu

Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,MarianExit
Chorus

{ Ni nani mwanadamu mwenye nguvu kuliko Mungu (hakuna) } *2

Ajitokeze mbele za watu tumuone, hakuna

Iyelele iyele, iyelele iyele - hakuna *4

Ni Mungu tu awezaye yote hivyo tumwogope

Verse 2

Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote

Analopanga Mungu mwanadamu halipangui

Akipanga uwe padri, utakuwa wewe padri

Akipanga we mtawa, utakuwa we mtawa, muogope Mungu

Verse 3

Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote

Analopanga Mungu mwanadamu halipangui

Akipanga uwe raisi, utakuwa we rais

Akipanga uwe waziri, basi wewe ni waziri, muogope Mungu

Verse 4

Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote

Analopanga Mungu mwanadamu halipangui

Akipanga uwe mbunge, basi wewe ni mbunge

Akipanga uwe balozi, utakuwa we balozi, muogope Mungu

Verse 5

Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote

Analopanga Mungu mwanadamu halipangui

Akipanga uwe tajiri, basi wewe ni tajiri

Akipanga uwe maskini, utakuwa maskini, muogope Mungu

Verse 6

Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote

Analopanga Mungu mwanadamu halipangui

Akipanga kukurudisha, mavumbini utarudi

Analopanga Mwenyezi, daima halipingiki, muogope Mungun