Verse 1
Tumpende tumsifu Mungu wetu wa milele na hata milele
Tulisifu jina lake tukufu, na kulitangaza ulimwenguni
Chorus
{Tumsifu daima kwa heshima nyingi
Ni Mungu kweli nasi tumsujudie } *2
Verse 3
Duniani hapasimami, ni pahali pa kuiweka miguu yake
Mbinguni ndipo aketipo , akiwaangalia wanadamu
Verse 4
Azishikaye mbingu na mawingu, zikae imara zisidondoke
Aupimaye mchana usizidi, wala usiku usididimike
Verse 5
Ailindaye mimea ya jangwani, pasipo mvua wala maji mengi
Azifanyaye bahari zidumu, hayo maji yake yasikauke