SectionsExitTumsifu Mungu

Tumsifu Mungu

Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,MarianExit
Verse 1

Tumpende tumsifu Mungu wetu wa milele na hata milele

Tulisifu jina lake tukufu, na kulitangaza ulimwenguni

Chorus

{Tumsifu daima kwa heshima nyingi

Ni Mungu kweli nasi tumsujudie } *2

Verse 3

Duniani hapasimami, ni pahali pa kuiweka miguu yake

Mbinguni ndipo aketipo , akiwaangalia wanadamu

Verse 4

Azishikaye mbingu na mawingu, zikae imara zisidondoke

Aupimaye mchana usizidi, wala usiku usididimike

Verse 5

Ailindaye mimea ya jangwani, pasipo mvua wala maji mengi

Azifanyaye bahari zidumu, hayo maji yake yasikauke