SectionsExitTumkimbie Shetani

Tumkimbie Shetani

Ordinary TimeExit
Chorus

Tumkimbie (tumkimbie) huyo huyo shetani (kimbia)

Shetani ameleta mafarakano katika dunia hii *2

Chuki zimetawala ee Bwana, magonjwa ni mengi sana

Tufanye nini tuepuke na matatizo haya *2

Verse 2

Tumeyasahau maagizo ya Bwana wetu Yesu Kristu

Aliyotufundisha sisi wanadamu, Ndiyo maana kuna machafuko

Verse 3

Mwenye masikio na ayasikilize maneno ya Bwana

Mkatende kama alivyotenda yeye, Dunia itakuwa na amani

Verse 4

Tungeishi na amani kama samaki katika bahari

Dunia hii ingekuwa ni paradise, Kama bustani ile ya Edeni

Verse 5

Tumelia sana Bwana hata machozi hayatoki tena

Tufanye nini sisi ni viumbe wako, Njoo haraka utusaidie