{ Tumesisimka (kweli) tunakuja kwako ee Baba
Tumeandama (sote) tunaleta zawadi zetu
Waumini wote simameni twende pamoja,
Tupeleke fedha mavuno na mifugo yetu } *2
Ondokeni Baba na mama ondokeni nanyi watoto
Chukueni fedha na mali, tupeleke mbele za Bwana
Tuweke akiba mbinguni, nasi tutabarikiwa *2
Hima hima twende pamoja, hima hima twende kwa Bwana
Tupeleke furaha zetu, tupeleke uchungu wetu
Simameni twende kwa Bwana tupeleke nyoyo zetun
Fedha za mifukoni mwetu tupeleke kwa ukarimu
Na mapato ya nguvu zetu, tupeleke kama zawadi
Twende kwake tumshukuru, sote tupate Baraka*2
Mavuno tuliyojaliwa, kutokana na jasho letu
Mifugo tunaowafuga, tupeleke kama sadaka
Tutabarikiwa zaidi, Bwana atatubariki *2n
Mkate mazao ya ngano, divai tunda la zabibu,
Kageuza mwili na damu, tutakula na kubakisha,
Tutapata nguvu zaidi, na uzima wa milele *2