SectionsExitTumaini Jema

Tumaini Jema

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Christmas,Christmas,Ordinary Time,Marian,Ordinary TimeExit
Verse 1

Hawataaibika, wala hawatafedheheka

Milele na milele (milele) wao watashinda magumu

Radi haitawapiga, mvua haitawagharikisha

Milele na milele (milele) wao watashinda mauti

Chorus

Tazama

Hawa ndio wale waliotambua (kuwa)

Bwana Yesu ndiye fimbo ya ushindi (tena)

Na wakakubali kumtumainia (yeye)

Yesu ni mwamba na yeye mshindi (ni)

Yesu kamanda wa wote tumwende yeye

Verse 3

Wamtumainiao, wamechagua fungu jema

Kwani hawatakwama wala kushindwa na lolote

Verse 4

Yesu aliahidi, kutoa kila aombwapo

Naye ni mwaminifu, anayetimiza ahadin

Verse 5

Kuugua kufiwa, si tatizo kwa watu hawa

Ufukara si hoja, kwa wamtumainiao Yesu

Verse 6

Vita wameshavishinda, mapambano wamemaliza

Na wamevikwa taji, wamevikwa taji la haki