SectionsBible ProcessionTulihubirije Neno

Tulihubirije Neno

Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Easter,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Christmas,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,MarianBible Procession
Chorus

Tutalihubirije neno lake Mungu

Huku viunoni mwetu ni mahirizi

Neno la Mungu halifanyiwi dhihaka

Tukaeni tukilijua jambo hili

Tuzitoe hirizi viunoni mwetu

Na vibuyu vilivyomo ndani ya nyumba

Tuuteketezeni ufalme wa giza

Tuukaribishe ufalme wa Mbinguni

Sikieni niwaambie siri moja

Ushirikina mwisho wake jehanamu

Tukikabidhi maisha yetu kwa Mungu

Tutapata mema na raha ya mbinguni

Verse 2

Ukitazama baadhi ya familia

Waziamini tunguri kuliko Mungu

Ukitazama baadhi ya familia

Wanaendesha kazi zao kwa tungurin

Verse 3

Wakati wengine wanapoenda ibada

Sisi wengine tunakwenda kunywa pombe

Kutokana na malezi yao nyumbani

Na watoto disko kulisakata rumba

Verse 4

Ndugu zangu sasa ninawakaribisha

Tuingie ndani ya hekalu ya Mungu

Kabidhi kila kitu kwake Mungu Baba

Mungu Baba ndiye mwisho wa mambo yote