Chorus
Tukuzeni Jina lake, milele na milele *2
Hubirini kwa watu ajabu zake zote
Semeni Bwana Mungu ni Bwana wa mabwanan{ Tangazeni kwa kuimba, kwa zaburi hata vinanda,
Na tarumbeta pia vinubi vyenye sauti ya kupendeza
Semeni ya kuwa ni Mfalme wa wafalme } *2
Verse 2
Mpeni Bwana utukufu,
Na nguvu pia mpeni, mwabuduni kwa uzuri wake,
Kwa uzuri wa utakatifu, tetemekeeni mbele zake
Verse 3
Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Mwimbieni Bwana wimbo mpya kwa maana ametenda
Ametenda mambo ya ajabu machoni pa mataifa
Verse 4
Paazeni sauti zenu,
Mkiimba kwa furaha, kwa madaha ukirukaruka
Ukicheza na kusimulia matendo yake ya ajabu