Tuidhihirishe Imani

Ordinary Time,Advent,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Lent,Ordinary Time,Marian,Christmas,Ordinary Time,Ordinary TimePrayers of the Faithful
Chorus

Waamini tunaalikwa, kuidhihirisha imani yetu kwa matendon{Ni mwaliko wa Baba Mtakatifu, ni mwaliko wa Kanisa

Kuipa uhai imani tunayoikiri,nimani tunayoiadhimisha, imani tunayoiishi } * 2

Verse 2

Imani tunayoikiri,

Ndiyo kusadiki kwa Mungu mmoja mwumba Mbingu na nchi

Ndiyo kusadiki kwa Bwana mmoja Yesu Kristu

Ndiyo kusadiki kwa Roho Mtakatifu

Verse 3

Imani tunayoikiri,

Ndiyo kusadiki kwa kanisa moja takatifu Katoliki la mitume

Kuungama ubatizo mmoja, ufufuko wa wafu na uzima wa milele

Verse 4

Imani tunayoadhimisha, ndiyo sakramenti za kanisa

Zilizo chemichemi za neema tupatazo kwa Mungu

Sisi tunaomwamini Kristu na kumfuata

Verse 5

Imani tunayoiishi, ndiyo kuziweka maishani mwetu amri zote za Mungu

Bila kuyumbishwa na hisia za uhuru wa kidunia

Na kubaki katika mtazamo wa Kimungu kwa mafundisho ya kanisa