SectionsExitTu Mavumbi Sisi

Tu Mavumbi Sisi

Ordinary Time,Advent,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,LentExit
Chorus

{ Siku zinapita, miaka yapita

Neno lake Bwana halitapita kamwe }*2

Chorus

Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini *2

Verse 3

mmmm mmmm mmm siku hiyo ni ya huzuni mnonmmmm mmmm mmm siku hiyo kweli inatisha

Verse 4

Kwa maana siku hiyo,

Mavazi yako yatakuwa ni sanda

Kitanda chako kitakuwa jeneza

Na nyumba yako iyakuwa kaburi

Jamaa zako watakutupia udongo,nkwa heri ya milele!

Chorus

Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini *2n{ Roho ndiyo roho ndiyo itiayo uzima

Mwili haufai kitu } * 2

Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini

Verse 6

Tazameni mimea, shambani

Matunda na maua, vyapendeza

Vyote vitanyauka

Wanyama wa pori, na nyumbani

Na ndege angani, wapendeza

Wote wataangamia

Verse 7

Ee ndugu sasa utubu rudi

Mrudie Mungu wako

Kwa maana duniani sisi ni wasafiri

Hujui saa na siku ndugu ya kuiacha dunia

Kwa maana duniani sisi ni wasafiri

Verse 8

Sayari angani zapendeza

Mito na mabonde duniani

Vyote vitatokomea

Mungu ndiye peke ajuaye

Siri ya maisha ya viumbe

Vyake ulimwenguni

Verse 9

{ Siku zinapita, miaka yapita

Neno lake Bwana halitapita kamwe }*2

Tu mavumbi sisi, tutarudi mavumbini * 2