Tazameni uwinguni, tazameni Mbinguni kwa Baba
Anakuja mtawala anakuja Bwana wa majeshi
Anakuja na hukumu zake na ujira wake mikononi
Anakuja duniani kote atawale mataifa
Yesu - ni Bwana wa mabwana,
Ni Mungu wa miungu
Mfalme Yesu, ni mfalme milele *2
Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba
Anakuja mhubiri anakuja mtabiri wetu
Anakuja na maneno yote ya kitabu chake mkononi
Anakuja ayasome yote yatokaye kwake Mungu
Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba
Anakuja daktari anakuja mwenye kutuponya
Anakuja mwenye matibabu na madawa yake mikononi
Anakuja awatibu wote wagonjwa wapate afya
Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba
Anakuja mchungaji anakuja mwana wake Mungu
Anakuja mchungaji mwema ana fimbo yake mkononi
Anakuja na malisho mema kwa kondoo wake wote.
Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba
Anakuja Mkombozi anakuja mwenye mamlaka
Anakuja na uhuru wake na funguo zake mikononi
Anakuja na kuwafungua wale wote walofungwa