SectionsExitTazameni Uwingu

Tazameni Uwingu

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Christmas,Advent,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,AdventExit
Verse 1

Tazameni uwinguni, tazameni Mbinguni kwa Baba

Anakuja mtawala anakuja Bwana wa majeshi

Anakuja na hukumu zake na ujira wake mikononi

Anakuja duniani kote atawale mataifa

Chorus

Yesu - ni Bwana wa mabwana,

Ni Mungu wa miungu

Mfalme Yesu, ni mfalme milele *2

Verse 3

Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba

Anakuja mhubiri anakuja mtabiri wetu

Anakuja na maneno yote ya kitabu chake mkononi

Anakuja ayasome yote yatokaye kwake Mungun

Verse 4

Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba

Anakuja daktari anakuja mwenye kutuponya

Anakuja mwenye matibabu na madawa yake mikononi

Anakuja awatibu wote wagonjwa wapate afya

Verse 5

Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba

Anakuja mchungaji anakuja mwana wake Mungu

Anakuja mchungaji mwema ana fimbo yake mkononi

Anakuja na malisho mema kwa kondoo wake wote.

Verse 6

Tazameni uwinguni, tazameni mbinguni kwa Baba

Anakuja Mkombozi anakuja mwenye mamlaka

Anakuja na uhuru wake na funguo zake mikononi

Anakuja na kuwafungua wale wote walofungwa