Chorus
Tazameni meza ya Bwana, inapendeza (kama nini)
Bwana Yesu ameandaa leo karamu kubwa (kweli kweli)
Ni chakula chenye uzima chakula cha roho *2
Verse 2
Bwana alivyo mkarimu kautoa mwili wake
Kautoa kama chakula cha wokovu wetu
Verse 3
Mwili wa Bwana Yesu ni chakula ni chakula bora cha uzima
Damu yake Bwana Yesu ni kinywaji cha kweli
Verse 4
Bwana ametualika, sote tujongee mezani
Tukale chakula cha uzima wa roho zetu