Tazama Ninakuja Kwako
Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Christmas,Advent,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,MarianBible Procession
Chorus
Tazama ninakuja kwako (Bwana),
Niyafanye mapenzi yako
Mimi ninajitoa kwako,nnaja kwako Bwana nipokee x2
Verse 2
Nimesikia Bwana, sauti yako yaniita kwako,
Yaniita nije kwako ili nikakutumikie.
Na mimi sina budi, kuitika wito wako,
Maana kila siku mimi hukutafuta wewe.
Verse 3
Naja kwako Bwana, nimejawa na furaha tele,
Nafsi yangu yashangilia kwa kuikaribisha kwako.
Na moyo wangu Bwana unakutukuza wewe,
Maana wastahili sifa zote pia utukufu.
Verse 4
Tazama naja kwako, ninayaleta maombi yangu,
Na sala zangu zote ninakuomba uzipokee.
Unisamehe dhambi na maovu niliyoyatenda,
Ili mimi niwe tayari kukupa sadaka takatifu
Verse 5
Ninajitoa kwako kuyatenda mapenzi yako,
Kwa nguvu zangu zote, kwa mawazo pia kwa vitendo,
Unijalie heri, unipe Roho Mtakatifu,
Aniongoze mimi, nitimize ninayoahidi.