Mwenyezi Mungu Rahimu na mradhi mwema,nsalamu salamu Mwumba wa Adamu
Watanzania tumekuja kwa wimbo,nna tenzi kuongea nawe leo hii
Uchaguzi mkuu huu tunaoandaa,ntwaomba ujae baraka zako kuu
Kusudi uwepo wako udhihirike,nkatika serikali tutakayounda
Rais mpya awe fimbo bora,nawe taa ya kweli kwenye kinara
Wabunge wawe matawi mazuri,nyenye kuzaa kwenye mti wa rutuba
Madiwani wawe watu wa watu,nkuongoza watu kwa ajili ya watu
Tujenge Tanzania madhubuti,nmioyoni badala ya ardhini
Wagonjwa wapone, makiwa wafarijiwe,nmasikini waonje maziwa kila siku
Wajane waishi, yatima waende shule,nfukara waone thamani ya utu wao
Majanga yakome, majeruhi watibiwe,nwalio gerezani wawe huru mitaani
Undugu ukue, amani iongezeke,nna wahalifu wote wabadilishe tabia
Na watoto, watoto wadogo,nwalelewe kwa maadili
Madhehebu, yote ya kidini,nyawe tahadhari ya upendo
Navyo vyama, vyetu vya siasa,nviwe siri kuu ya amani
Ibilisi, afunge virago,naondoke kamwe asirudi!n
Kiapo atakachoapa rais mpya,nkidumu hata hatimamu ya dahari
Majaribu yote yatakayotukumbuka,nyapimwe yasizidi kimo chetu
Mwenyezi Mungu rahimu twakuomba,ntulinde tulinde bila ya kuchoka
Ili mwisho wa safari ya hapa,ntufike mbinguni wote Tanzania