Chorus
{ Talanta tulizopewa na Mungu (Mwenyezi)
Tuzitumieni kwa kujipatia utakatifu } *2
Verse 2
Kama wewe ni baba wa familia
Au kama wewe ni mama wa familia
Kama wewe ni kasisi kanisani
Au kama wewe mtawa kanisani
Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
Verse 3
Kama wewe ni hakimu toa haki
Au kama wewe askari tenda haki
Usionee wanyonge masikini
Acha rushwa acha dhuluma tenda haki,
Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
Verse 4
Kama wewe dakitari au nesi
Hudumia wagonjwa wote kwa upendo
Mashambani maofisini wajibika
Acha uvivu fanya kazi kwa bidii,
Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu*2
Verse 5
Viongozi na watawala tenda haki
Kumbukeni mtaulizwa na Muumba
Walimu nanyi fundisheni maadili
Nanyi wafanya biashara tenda haki
Tutaulizwa juu ya talanta alizotupa Muumba *2