Chorus
Sote tusimame kwa heshima ya jina la Bwana
Tumwimbie Mungu wimbo mpya ule wa masifu
Kwa vinanda hata na vinubi tumwimbie
Mungu wetu aliyetuumba, ni Baba wa mababu zetu
Verse 2
Tupige vigelegele, tupigeni na makofi
Sisi tumekombolewa, tuimbe tushangilie
Verse 3
Kaigeuza bahari, ikawa nchi kavu,
Njooni tuyasimulie, matendo ya Mungu wetu
Verse 4
Alikemea bahari, mawimbi yakanyamaza
Mungu wetu ni mkuu, jina lake litukuzwe