SectionsExitSitawaacha Nyinyi

Sitawaacha Nyinyi

Exit
Chorus

Sitawaacha nyinyi kama yatima,

Sitawaacha nyinyi (Acha nyinyi) asema

Bwana (ee Bwana) (Naja kwenu mioyonyenu ijae, furaha na amani,

Asema Bwana) *2 eeh

Verse 2

Nitawaombea nyinyi kwa Baba yangu

Naye atamtuma Roho wa kweli

Huyo Roho Baba atakayemtuma

Ndiye atakayewafariji mioyoni

Verse 3

Utukufu ulionipa ee Baba

Nimewapa na wao ili wapate

Kujua ndiwe peke uliyenituma

Ukawapenda wao ulivyonipenda

Verse 4

Baba hao ulionipa nataka

Wawe pamoja nami, nami popote

Popote kutazama utukufu wako

Utukufu ulionipa, anasema Bwana

Verse 5

Baba si hao tu ninawaombea

Lakini nao wale wataoniamini

Wote wawe umoja kama we Baba

Ulivyo ndani yangu nami ndani yako

Verse 6

Sitawaacha nyinyi kama yatima

Waipeleka roho, yako e Baba

Nawe unaufanya uso wa nchi

Uso wa nchi upya, anasema Bwana